Mhe. Rais, Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania, ni muungano wa mashirika zaidi ya
100 yanayo tetea haki za binadamu Tanzania. Mtandao kwa kushirikiana na Wanachama wake pamoja
na wasio wanachama tumehuzunishwa na kitendo cha Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitisha
Muswada wa Sheria ya Takwimu ya Mwaka 2015 na Muswaada wa Sheria ya Makosa ya Mtandaoni
bila kuviondoa vifungu vinavyokwenda kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya
mwaka 1977 na Haki za Binadamu kwa Ujumla.
Tunafahamu kabisa dhamira yako ya kuhakishia watanzania wanapata uhuru wa maoni na uhuru wa
kufanya shughuli zenye tija kwa Taifa kwa uhuru. Pia tunatumia fursa hii kukupongeza Mhe. Rais Kw
kwa jitihada za kuongeza wigo wa ushiriki wa wadau katika mambo mbalimbali kwa kuanzisha
progamu mbalimbali za utawala bora, uwazi na ukweli kama vile Open Government Partnership na
mengineyo. Kwa misingi hiyo Mheshimiwa Rais, tunashauri kabla ya kutia saini miswaada hii upate
muda wa kusikiliza kilio cha jamii juu ya ubaya wa sheria hizi kwa mustakabali wa Taifa. Sheria Hizi
zikitumika katika utwawala wako zitatia shaka dhamira yako nzuri ambayo umekuwa ukisimamia toka
uingie madarakani ya kuongeza wigo na uhuru wa habari na ushiriki wa wadau katika maendeleo ya
kitaifa.
Soma zaidi...Sikika
No comments:
Post a Comment