Sunday, August 28, 2016

Sikika yafanya mkutano wa wadau wa afya wa kuhimiza Ufuatiliaji wa Uwajibikaji Jamii (SAM) Wilayani Kilolo

Mkurugenzi wa Sikika Bw. Irenei Kiria (wa kwanza kushoto) akifanya utambulisho katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo kabla ya kuanza kwa  mkutano wa wadau wa afya wilayani Kilolo. Lengo la mkutano huo ni kuwasilisha matokeo ya zoezi la SAM lililofanyika wilayani humo.
Afisa Mipango wa wilaya ya Kilolo Bw. Jasphone Mukungu akikaribisha wadau wa afya katika mkutano huo.
Afisa programu kutoka Sikika Bw. Hendry Samky akitambulisha wadau mbalimbali wa afya.

Bw. Irenei Kiria akitoa neno la shukrani.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo Bw. Aloyce Kwezi akisoma hotuba mbele ya waandishi wa habari na wadau wa afya (hawapo pichani).
Mjumbe wa timu ya SAM Bi. Rehema Msola akiwasilisha matokea ya zoezi la SAM. 

Baadhi ya wadau wa afya wakifuatilia akiwasilishaji wa matokea ya zoezi la SAM wilayani Kilolo. 
Mjumbe wa SAM Bw. Amos Lugwago akiwasilisha matokea ya zoezi la SAM katika picha.
Mganga Mkuu wa wilaya ya Kilolo Dkt. Mohamedi Mang'una akitoa muongozo wa ratiba katika mkutano huo.
Timu ya SAM na wadau wa afya katika picha ya pamoja.
Timu ya SAM katika picha ya pamoja na mgeni rasmi (wa saba kutoka kulia).

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Wajumbe wa Kamati za Usimamizi wa Vituo vya huduma za afya katika picha ya pamoja.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo Bw. Valence Kihwaga akiongea na baadhi ya waandishi wa habari. 
Mwenyekiti wa timu ya SAM wilaya ya Kilolo Bw. John Kasuga akitoa neno la shukrani mbele ya wadau wa afya (hawapo pichani).
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo Bw. Valence Kihwaga akifunga mkutano wa wadau wa afya wilayani Kilolo.


No comments: