Thursday, September 22, 2016

Timu ya SAM yawasilisha taarifa ya awali kwa watendaji wa Halmashauri wilayani Kondoa

Mwenyekiti wa timu ya SAM wilayani Kondoa Bw. Mohamed Thawa akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya manispaa ya Kondoa Bw. Kibasa Falesy Mohamed katika mkutano wa ndani (Internal Meeting). Lengo la mkutano huo ni kuwasilisha matokeo ya awali kwa watendaji wa Halmashauri hiyo ili kutoa fursa kwa ajili ya ufafanuzi. Kushoto ni Mkuu wa programu za Afya - Sikika Bi. Alice Monyo. 
Bw. Kibasa Falesy Mohamed akizungumza katika mkutano huo.  

Bw. Mohamed Thawa akipokea baadhi ya nyaraka kutoka kwa Timu ya Utawala wa Afya ya Halmashauri (CHMT) kwa ajili ya majadiliano.
Timu ya Utawala wa Afya ya Halmashauri (CHMT).  
Mratibu wa Sikika wilayani Kondoa Bw. Nelson Lema akitoa utambulisho.  

Mjumbe wa timu ya SAM Bi. Shakila Ibrahim (Kushoto) akifafanua hoja. Kulia ni Mh. Mtendaji Mwanaisha Maiwa.

Mjumbe wa timu ya SAM Ally Kisele akiomba ufafanuzi wa kina kuhusu ujenzi wa wodi katika hospitali ya wilaya.  
Mjumbe wa timu ya SAM, Mh. Bashiru akitaka ufafanuzi zaidi juu ya hoja zilizowasilishwa. 
Katibu Mkuu wa wilaya ya Kondoa Bw. Alpha Cholobi akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja.
Mganga Mkuu wa wilaya ya Kondoa Dk. Rashid Ikaji akitoa ufafanuzi wa hoja zilizotolewa na timu ya SAM. 
Bw. Kibasa Falesy Mohamed akiagana na wajumbe wa timu ya SAM baada ya Mkutano. 

No comments: