Thursday, July 17, 2014

Sikika yafanya mkutano wa kwanza na wadau wa Afya wilayani Kondoa, ikiwa ni hatua ya awali ya zoezi la SAM 2014

Mratibu wa Sikika wilayani Kondoa Bw. Nelson Lema akitambulisha wadau mbalimbali wa afya walioalikwa katika  mkutano wa kwanza wa wadau wa afya wilayani humo (Kushoto) ni Katibu tawala wa wilaya Bi. Winnie Kijazi.
Katibu tawala wa wilaya ya Kondoa Bi. Winnie Kijazi akisoma hotuba katika mkutano wa kwanza wa wadau wa afya wilayani humo. (Kulia) ni Mratibu wa Sikika wilayani Kondoa Bw. Nelson Lema na (Kushoto) ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Emmanuel Sekwao. 
 Makamu Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Kondoa Bw. Juma N. Hapi akiahidi kutoa ushirikiano kwa timu ya SAM wilayani humo.
Mratibu kutoka Sikika Bw. Zakayo Mahindi akiwasilisha mada ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii (SAM) katika mkutano wa Wadau wa Afya wilayani Kondoa.
Mratibu kutoka Sikika Bw. Fredrick Ngao (aliesimama)  akitoa utangulizi katika mkutano huo.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Dkt. Karume Maisala akichangia jambo katika mkutano huo. 
Kutoka Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa Bw. Emmauel Sekwao na Katibu tawala wa wilaya hiyo  Bi. Winnie Kijazi wakifuatilia kwa umakini uwasilishaji wa mada katika mkutano huo. 
Wadau mbalimbali wa Afya wilayani Kondoa wakifuatilia mjadala kwa makini katika mkutano huo. 
Wajumbe wa timu ya SAM wilayani Kondoa wakimpongeza Mwenyekiti wa timu hiyo mara baada ya kuchaguliwa. 
Wajumbe wapya wa timu ya SAM wilayani Kondoa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano kumalizika.

No comments: