Kamati
hiyo ya Bunge iliomba kukutana na Sikika kufuatia tamko la Shirika kuhusu kuishauri
serikali na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha hatua za
mwanzo za uandaaji wa bajeti za serikali unakua na umakini mkubwa ili kuepuka
kusababisha mianya inayoweza kupelekea bajeti kuwa na matumizi yasiyo ya lazima
yanayoweza kusababisha ufujaji wa fedha za umma.
Lengo
la kamati hii ya bunge kutaka kukutana na wadau wa sekta ya afya ni kupata uzoefu
na uelewa zaidi kabla ya kukutana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na watoto, Mh. Ummy Mwalimu.
Kati
ya mambo makuu yaliyojadiliwa ni: Utendaji kazi wa Sikika, Sekta ya Afya na
changamoto zake, pamoja na mfumo wa Mgawanyo wa Bajeti.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma na
Maendeleo ya Jamii, Dk. Raphael Chegeni akifungua mjadala kati ya Sikika na
kamati hiyo ya Bunge. (Pembeni yake ni Katibu wa kamati hiyo
ya Bunge).
Dk. Raphael Chegeni akionyesha gazeti lililoituhumu kamati hiyo
kwa ufisadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Sikika, Bw. Irenei Kiria akielezea Kamati
ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii juu ya Shirika na namna linavyofanya
kazi katika sekta ya afya nchini ili kutetea upatikanaji wa huduma bora za Afya kwa kila mtu.
Mkuu wa Idara ya Dawa
na Vifaa Tiba wa shirika la Sikika, Bi.
Alice Monyo akielezea juu ya umuhimu wa sekta ya afya na changamoto mbalimbali
zinazoikumba sekta hiyo.
Dk. Wilson Kitinya kutoka Sikika akitoa mada juu ya mfumo wa mgawanyo wa bajeti.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati kuanzia kushoto Mh. Dr. Charles
Tzeba (CCM-Buchosa), Mh. Juma Nkamia (CCM-Kondoa), Kabwe Zuberi Zitto (ACT-Kigoma
Mjini) wakifuatilia mjadala.
| Mh. Kabwe Zuberi Zitto akichangia mada. |
| Mh. Dr. Charles
Tzeba akiuliza swali juu ya mgawanyo wa watumishi wa afya nchini, mojawapo likiwa ni kutaka kujua kwanini watumishi wa afya wapo wengi Kinondoni lakini hawapo Singida...? |
Mbunge wa Viti Maalum, Mh. Jacqueline Kandidus Ngonyani (CCM) akichangia jambo.
Mbunge wa Buyungu Mhe. Kasuku Samson Bilango (CCM) akielezea kwa uchungu vifo vya mama
wajawazito pamoja na kukosekana kwa
magari ya huduma za wagonjwa (ambulance).
Mbunge wa Nzega (CCM) Mh. Hussein Bashe akiuliza maswali, mojawapo
likiwa ni kutaka kujua kama Sikika huwa inafuatilia iwapo dawa zinazoandikwa
kupelekwa katika vituo vya afya huwa zinafikishwa eneo husika au la kutokana na
tatizo sugu la kukosekana kwa dawa katika vituo vya afya.
Mbunge wa Viti Maalum, Mh. Susan Anselm Jerome (Chadema)
akifuatilia mjadala kati ya Sikika na kamati ya bunge wakifuatilia mjadala.
| Baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia mjadala. |
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Sikika akijibu swali la mjumbe
wa Kamati Mh. Juma Nkamia (wa kwanza kulia) juu ya shirika la Sikika kuwa
lina bajeti kiasi gani, linapata wapi pesa ya kujiendesha, wafadhili
wake ni wakina nani na kama shirika linafanya ukaguzi wa mahesabu.
Mkuu wa Idara za Sikika Bw. Patrick Kinemo
akielezea sababu mbalimbali zinazosababisha vifo vya akina mama na watoto.
Dk. Wilson Kitinya kutoka Sikika akifafanua jambo katika
mkutano huo.
No comments:
Post a Comment